SUBSCRIBE NOW: /user/uwazi1
Dunia imekwisha! Baba Anaswa Gesti na Binti yake wa Kumzaa Mwenyewe. Fadhil Mshamu, mkazi wa Kibaha Kwa Mfipa mkoani Pwani, Julai 27, 2017 alikumbwa na aibu kubwa, baada ya kubambwa na polisi, akidaiwa kumshawishi binti yake wa kumzaa ili ampe penzi.
UANZE MKASA HUU KWA UMAKINI
Kitengo Maalum cha Oparesheni Fichua Maovu (OFM) cha Global Publishers, mwanzoni mwa wiki hii kilipokea simu kutoka kwa mwanamke mmoja, aliyedai wanahitaji msaada kwani katika familia yao, kuna tatizo kubwa ambalo limewasumbua kwa muda mrefu.
Mwanamke huyo aliyedai anaishi Buguruni jijini Dar es Salaam, alipotakiwa kudokeza tatizo hilo, alidai kuwa katika familia yao, kuna baba anataka kuvunja amri ya sita na binti yake!
OFM WASHTUKA, WATUA BUGURUNI
Kwa taarifa hiyo ya kushtusha, makamanda wa OFM walilazimika kufika Buguruni ili kupata habari kamili na kufika huko, walikutana na mwanamke aitwaye Tatu Mshamu waliyezungumza naye kwa simu, ambaye alijitambulisha kama shangazi wa binti anayetakiwa kutenda dhambi hiyo na baba yake!
FACEBOOK: https://www.facebook.com/Globalpublishers/
TWITTER: https://twitter.com/GlobalHabari
Visit https://globalpublishers.co.tz/, Subscribe /c/uwazi1
Kupata video nyingine za aina hii, subscribe kwenye chanell yetu kwa kubofya…
/c/uwazi1
HUYU HAPA SHANGAZI
“Huyu ni mtoto wa kaka yangu, kila siku anatuambia baba yake anamsumbua, anamtaka kimapenzi. Tumejaribu kukaa naye na kuzungumza, lakini anatuambia watoto wanamsingizia tu, siyo kweli. Tunajiuliza kwa nini kila siku wakusingizie wewe tu?
“Sasa leo tukaona labda kweli hawa watoto huenda wana lao jambo, tukamwambia huyu binti, hebu tuthibitishie kama unachoongea ni cha kweli, akasema ngoja apige simu kwa baba yake, akaweka laudi spika!
“Akampigia mbele yetu, tukawa tunamsikia anavyombembeleza. Sasa sisi tumechoka, tunataka hili jambo bora lijulikane, maana tumezungumza naye haelewi, kama mbwai na iwe mbwai tu!”
WASOMBWA POLISI
Kufuatia sakata hilo, maafande hao waliwachukua mama, shangazi, binti huyo na baba yake na kuwapeleka Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Kibaha ambapo baada ya mahojiano walimfungulia jadala la uchunguzi lenye namba KBA/RB/4067/2017.
Baadaye baba huyo alihamishiwa Kituo Kikuu cha Mkoa na kufunguliwa jalada lingine lenye namba KBA/IR/2278/2017
FACEBOOK: https://www.facebook.com/Globalpublishers/
TWITTER: https://twitter.com/GlobalHabari
Visit https://globalpublishers.co.tz/, Subscribe /c/uwazi1
Kupata video nyingine za aina hii, subscribe kwenye chanell yetu kwa kubofya…
/c/uwazi1/c/uwazi1/c/uwazi1
WEBSITE: https://globalpublishers.co.tz/
FACEBOOK: https://www.facebook.com/Globalpublis ...
TWITTER: https://twitter.com/GlobalHabari
INSTAGRAM: https://www.instagram.com/globalpubli ...