المدة الزمنية 7:28

SILINDE AAGIZA WALIMU WAKUU WAWILI KUCHUNGUZWA NA TAKUKURU

بواسطة Millard Ayo
4 539 مشاهدة
0
18
تم نشره في 2021/01/13

Naibu waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI David Silinde ameagiza kuchunguzwa kwa miradi miwili ya ujenzi wa mabweni ya sekondari ya Mang'ola na shule ya Domel baada ya kuwa namashaka na matumizi mabaya ya fedha wakati wa ununuzi wa vifaa ambavyo vinatofautiana bei na zote zipo katika maeneo ya karibu lakini manunuzi ya vifaa hivyo vinatofautiana bei na kushindwa kumaliza majengo hayo kwa wakati baada ya fedha kuisha. Naibu waziri Silinde amechukua maamuzi hayo baada ya kufanya ziara ya ukaguzi katika wilaya karatu mkoa wa Arusha na kugundua ubadhilifu huo na kuagiza wakuu wawili hao wa shule kuandika barua ofisi ya Rais Tamisemi ya kwanini wasichukuliwe hatua za kinidhamu kwa kushindwa kusimamia miradi hiyo huku afisa elimu wa wilaya na mhandisi wa wilaya nao wakiagizwa kuandika barua ya kwanini wasichukuliwe hatua za kinidhamu. Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Karatu Abbas Kayanda amesema amepokea maagizo ya Naibu waziri na kwa kuanza alimuagiza kamanda wa TAKUKURU wilaya hiyo kuanza uchunguzi mara moja na kupelekewa taarifa mapema. Aidha Naibu waziri Silinde akitembelea wilaya ya Monduli na kuwapongeza baada ya miradi yote ya lipa kwa matokeo EP4R kumalizika tangu mwezi wa kumi mwaka jana na kuendana na maagizo ya serikali kuwataka wakamilishw ndani ya miezi mitatu na kwa ubora mnzuri.

الفئة

عرض المزيد

تعليقات - 6