Mkoa kaskazini Unguja..25/8/2021
Mkuu WA mkoa kaskazini Unguja Ayoub Mohamed Mahmoud, amesema sio Jambo la busara Kwa masheha kuwabagua na kuwakosesha huduma wananchi Kwa sababu ya tofauti zao binafsi.
Akizungumza na masheha afisini kwake mkokotoni amesema kumtenga mwananchi na kutompatia huduma stahiki ni kumkosesha haki yake ya msingi.
MH Ayoub amesema kazi ya usheha inahitaji busara na kuzingatia sheria za tawala za mikoa zinavyoelekeza katika utekelezaji wa majukumu Yao.
Baadhi ya masheha waliopatiwa mafunzo elekezi Ya kutambua majukumu Yao katika utoaji huduma Kwa wananchi, wamesema watahakikisha wanasimamia utatuzi wa migogoro ili kupata fursa ya kutekeleza shughuli za kimaendeleo.
الفئة
عرض المزيد
تعليقات - 0
مقاطع الفيديو ذات الصلة على MKUU WA MKOA WA KASKAZINI MH. AYOUB MOHAMED: