المدة الزمنية 4:11

MABALOZI WASTAAFU WAPIGA SALUTE UJENZI WA BWAWA LA MWALIMU NYERERE

بواسطة KONCEPT TV
401 مشاهدة
0
2
تم نشره في 2021/07/21

MABALOZI WASTAAFU WAKUBALI UJUZI WA WATANZANIA MRADI WA UMEME WA JULIUS NYERERE Mabalozi wastaafu wa Tanzania waliohudumia kwenye Nchi mbalimbali Duniani leo Julai 17, 2021 wametembele mradi wa kufua umeme kwa maji wa Julius Nyerere Mw 2115 (JNHPP). Akiongea katika ziara hiyo Mwenyekiti wa Mabalozi Wastaafu, Balozi Celestine Liundi amesema wametembelea JNHPP ili kuona kitu gani kinaendelea katika ujenzi wa bwawa la Nyerere. "Tumejionea sisi wenyewe jinsi gani Teknolojia inavyoweza kubadilisha mazingira, na tumeona Watanzania wamepata ujuzi kupitia mradi huu wa Julius Nyerere" amesema Balozi Liundi. Ameongeza ziara hiyo sio tu imewawezesha kuufahamu mradi wa Julius Nyerere bali pia mabalozi wamejifunza namna ambavyo Watanzania wamepata maarifa, uwezo na ujuzi. "kazi ya mabalozi ni diplomasia na kuwaunganishia watu, hivyo ziara hii itatuwezesha kutoa elimu kwa wengine ili lengo la kujenga uchumi imara wa Tanzania liweze kutimia" alisema Balozi Liundi. Mabalozi wameishukuru TANESCO kwa kuwapa fursa ya kufika kuona na kujifunza yanayoendelea katika mradi wa Julius Nyerere.

الفئة

عرض المزيد

تعليقات - 0