المدة الزمنية 4700

Rais Samia: Nataka niwe Mkweli, Kwasasa Hatutaweza

بواسطة JamiiForums
239 مشاهدة
0
0
تم نشره في 2021/06/29

Samia Suluhu Hassan, Rais - Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Vyombo vya Habari vina mchango mkubwa kulinda Umoja wa Kitaifa, Usalama Nchi, Kuchochea shughuli za maendeleo. Vinasaidia Kufichua Maovu kwenye Jamii ikiwemo uzembe kazini, rushwa na ubadhirifu wa mali za Umma Nawapongeza kwa kazi nzuri mnayoifanya kwa nchi yetu i. Vyombo vya habari kunyimwa matangazo Hili la Vyombo vya Habari kunyimwa matangazo, sijalikuta mezani kwangu Kuna ushindani katika kupata matangazo Kule Zanzibar tunayo Suluhu Network TV, mpaka leo mishahara tunachanga! Hatujapata matangazo ya kuendesha kituo ii. Madeni Suala la Madeni, nitashirikiana na Waziri Mkuu yalipwe kidogokidogo. Lakini lazima tuyahakiki kama ni madeni halali iii. Stimulus package Stimulus package kwaajili ya athari za #COVID19 kwakweli ni changamoto Tunaweza kuliangalia huko mbeleni, hata Uchumi wenyewe wa Taifa unapitia wakati mgumu iv. Leseni kulipiwa kwa Dola Suala la Leseni kulipwa kwa Dola hata nami naliona kuwa ni changamoto. Hatuwezi kuwa Watumwa wa Sheria tunazozitunga. Tutakaa kitako tuangalie tunakwendaje v. Kazi ya Urais Kazi ya Urais ni ngumu, lakini urais ni Taasisi Rais hafanyi kazi peke yake; ndani ya Ofisi yake kuna Wasaidizi kadhaa lakini si rahisi kihivyo. Inabidi ujue kila kitu kinachotokea, usome na utafute Inakuwa ngumu zaidi kama hukujipanga kuichukua vi. Siku 100 Madarakani Katika siku 100 nilizokaa madarakani, kuna ambayo nami nimesikia yamefanyika nami nikashangaa Tumehimili vishindo; thamani ya pesa yetu bado iko imara na mfumuko wa bei umedhibitika Tuna akiba ya takribani Dola Bilioni 4.97 hivyo uhakika wa kujiendesha miezi 6 upo vii. Idara ya Habari kwenda Wizara ya Teknolojia ya Habari Kuhusu pendekezo la Idara ya Habari iende kwenye Wizara ya Teknolojia ya Habari, tutakaa tuyaangalie kwa pamoja Tukiwa na 'justification' ya kutosha basi tunaweza tukaamua vinginevyo viii. Kukabiliana na Covid 19 Kuna wanaoona hatuko serious ktk mapambano dhidi ya Covid 19 Nilipoingia madarakani nilitamani tupambane na ugonjwa huu kama wanavyofanya mataifa mengine Tanzania tuna wagonjwa zaidi ya 100 wenye wimbi la tatu la Covid 19 Tumeamua tukubali chanjo kwa walio tayari Tanzania tumeingia kwenye COVAX community Wataalamu wetu wanafanyia kazi Chanjo ipi inafaa kwa Watanzania Kuna mashirika mengi wamejitokeza kutaka kusaidia Watanzania lakini lazima wataalamu wetu ndio watoe ushauri kitaalamu Mapambano ya Covid 19 si ya Serikali tu. Sisi kama Serikali tunahimiza yale yanayoshauriwa na wataalamu; kama unaamini kwenye kupiga nyungu - wewe piga. Kila mmoja atekeleze wajibu wake. Jikingeni sana na wakingeni watoto Tuna $470m za kuagiza chanjo na vifaa vya kupambana na Covid 19 ix. Teuzi za viongozi Kwenye teuzi hatuwezi kumchukua kila aliyesema “CCM OYEE” Kwenye teuzi kuna waliokuwa wapinzani, kuna wasiokuwa na vyama na hata wana CCM. None is left behind x. Uwekezaji nchini Wawekezaji waliosajiliwa kuanzia Machi hadi Mei ni mara mbili ya waliojitokeza kipindi kama hiki mwaka jana Naendelea kufungua milango ya kukuza uchumi xi. Katiba Mpya Naomba nipeni muda kwanza niisimamishe nchi kiuchumi halafu tutashughulikia mengine Tutashughulikia Katiba Mpya lakini Vyama vya Siasa viendelee kufanya Siasa kwenye maeneo yao Sisemi Katiba sio ya maana, ni ya maana sana

الفئة

عرض المزيد

تعليقات - 1