Subscribes:/c/KidaniStars
WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa ameipongeza Simba SC kwa kupata ushindi wa kwanza ugenini kwenye hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya AS Vita jana usiku Kinshasa, DR Congo.
Simba ilishinda bao 1-0 dhidi ya AS Vita kwa mkwaju wa penalti uliowekwa wavuni na Chris Mugalu dakika ya 60 na kuipa uhakika wa alama tatu timu yake.
Majaliwa ameyasema hayo wakati akiahirisha vikao vya Bunge jijini Dodoma na wabunge wakilipuka kwa furaha kushangilia.
"Nawapongeza pia mabingwa wa soka Tanzania timu ya Simba SC kwa kufanikiwa kufuzu hatua ya makundi na jana kushinda mchezo wake wa kwanza ugenini dhidi ya AS Vita nchini DR Congo," amesema Majaliwa
Waziri Mkuu pia amempongeza Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzalez kwa ubunifu wake wa kushirikisha Wizara ya Utalii na kuja na wazo la kuweka maneno ya 'Visit Tanzania' kwenye jezi za Simba ambazo zinazotumika katika hatua ya makundi kutokana na kanuni za CAF kutoruhusu kampuni za kubeti kutumika kwenye jezi za klabu.
HABARI MPYA DAILY:https://bit.ly/3c3bEDc
HABARI ZA MICHEZO: https://bit.ly/2TAgnWx
HABARIZA WASANII: https://bit.ly/2X2f84R
HABARI ZA SIASA: https://bit.ly/36r0xCW
Instagram: https://www.instagram.com/kidanistars
Facebook: https://www.instagram.com/kidanistars
Twitter: https://twitter.com/Kidanistars
Subscribes:/c/KidaniStars