Timu Feisal Salum, #TeamFeisal imeondoka na ubingwa wa penati 4-2 baada ya sare ya bao 1-1 dhidi ya Timu ya Abdulaziz makame #BuiCombine katika mchezo wa hisani wa kusaidia akina mama wajawazito #SaidiaWazazi uliochezwa leo kwenye Uwanja wa Mao, visiwani Zanzibar.
Team Feisal ilitangulia kupata bao kupitia kwa Matheo Anthony dakika ya 6 kabla ya Obrey Chirwa kuisawazishia Bui Combine dakika ya 89.
Ikapigwa mikwaju kumi ya penati ambapo Team Feisal ilipata penati nne ikiwemo y Fiston Mayele dhidi ya mbili za Bui Combine.
Tazama hapa magoli mawili na penati zote kumi.