Dar es Salaam. Mtoto wa Rais wa awamu ya tano hayati John Magufuli, Joseph Magufuli amesema mama yake anaendelea na matibabu baada ya kupatwa na mshtuko kufuatia kifo cha mumewe.
Akizungumza kwa niaba ya familia ya Magufuli wakati wa kongamano la viongozi wa dini, Joseph amesema mama Janeth hayuko vizuri kiafya na anaendelea na matibabu.