المدة الزمنية 5:44

USIYOYAJUA Kuhusu Ndege Aina ya Boeing 787 Dreamliner

بواسطة Global TV Online
48 230 مشاهدة
0
163
تم نشره في 2018/07/27

Usiyoyajua Kuhusu Boeing 787 Dreamliner Usiyoyajua Kuhusu Boeing 787 Dreamliner Machi 31, 2017, ndege aina ya Boeing 787 zilianza kutembea rasmi na ndege hizo zipo tatu tu, 787-8, 787-9 na 787-10. Boeing 787-8 ni ya nne kuwasili nchini kati ya saba zilizonunuliwa awali na serikali kwa ajili ya kuliwezesha Shirika la Ndege la Tanzania {ATCL} kuimarisha huduma zake. Uzuri wake Boeing, 787-8 Dreamliner ni familia yenye teknolojia ya kisasa, ndege hii ina utendaji mzuri na vitu vipya vya kupendeza ndani. Siti zake zipo katika mfumo wa siti 9 ambapo mgawanyo wake upo kwa 3-3-3 huku kila siti ikiwa na upana wa sentimeta 43.7, kwa ilivyotengenezwa, ina uwezo wa kuchukua abiria kuanzia 242 Mbali na kuleta vigezo vya ndege kubwa katika ndege za wastani, 787 Dreamliner italipatia shirika la ndege la Air Tanzania ufanisi wa mafuta na mazingira ya utendaji, kwa kutumia chini ya asilimia 20 hadi 25 ya mafuta na asilimia 20 hadi 25 wa uchafuzi wa mazingira ikilinganishwa ndege nyengine zilizotumika awali. Uwezo wake Ndege hii yenye urefu wa mita 56.7 na upana mita 5.9 ina uwezo wa kuhifadhi mafuta lita 126,210 huku ikiwa na uzito wa kilogramu 228,000. Ina kasi ya ajabu ambapo uwezo wake wa spidi ni maili 593 kwa saa na kilomita 954 kwa saa wakati injini yake inaitwa Rolls-Royce Trent 1000 yenye thamani ya dola za Kimarekani milioni 41 (zaidi ya bilioni 93 za Kitanzania). Thamani yake Boeing 787-8 thamani yake ni dola za Kimarekani milioni 224.6 (zaidi ya shilingi bilioni 509.5 za Kitanzania), wakati aina mbili nyingine za Boeing ni dola milioni 264.6 (zaidi ya bilioni 600 kwa Boeing 787-9 na dola milioni 306.1 (zaidi ya bilioni 694.4 za Kitanzania) kwa Boeing 787-10. Zilizowahi kununuliwa Ukiachana na Boeing 787-8, ndege nyingine ambazo zimeshanunuliwa chini ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli ni Bombardier Q400 Dash 8 NextGen , ndege mbili aina ya Bombardier CS300 zenye uwezo wa kuchukua kati ya abiria 137 na 150 . Masafa yake Ndege hizo zinafanya masafa baadhi ya mikoa nchini pamoja na nje ambayo ni Dodoma, Mwanza, Arusha, Mbeya, Kigoma, Tabora, Mpanda, Kilimanjaro, Mtwara, Zanzibar, Pemba, Bukoba na Visiwa vya Comoro. Install GlobalPublishersApp Android: http://bit.ly/2AAQe1d iOS: http://apple.co/2Assf4M Subscribe /c/uwazi FACEBOOK: https://www.facebook.com/Globalpublis ... TWITTER: https://twitter.com/GlobalHabari Visit https://globalpublishers.co.tz/, Suazi1 /c/uwazi1 WEBSITE: https://globalpublishers.co.tz/ FACEBOOK: https://www.facebook.com/Globalpublis ... TWITTER: https://twitter.com/GlobalHabari INSTAGRAM: https://www.instagram.com/globalpubli ..

الفئة

عرض المزيد

تعليقات - 7