المدة الزمنية 25:52

LIVE ​Tazama Mwitikio wa Jeshi la Kujenga Taifa Kwenye Kilimo cha Mkonge (835KJ MGAMBO TANGA)

بواسطة Ulinzi Channel
4 259 مشاهدة
0
33
تم نشره في 2021/11/03

JKT LAITIKIA WITO WA KILIMO CHA MKONGE eshi la Kujenga Taifa chini ya Mkuu wa Jeshi hilo Meja Jenerali Rajabu Mabele kupitia Kikosi cha 835 Mgambo JKT kilichopo Wilayani Handeni Mkoani Tanga limeitikia kwa vitendo kilimo cha zao la Mkonge/Katani. Kufuatia maelekezo ya Serikali yaliyotolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa yaliyozitaka Taasisi na Mashirika katika Mkoa wa Tanga kujikita kwenye kilimo cha zao la Kibiashara la Mkonge. Mkurugenzi wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Jeshi la Kujenga Taifa Kanali Peter Lushika ametembelea Kikosi hicho ili kujionea hatua iliyofikiwa ili kufikia malengo yaliyowekwa. Akizungumza kwenye eneo la mradi huo Kanali Peter Lushika ameridhishwa na hatua iliyofikiwa ambapo amejionea Mgambo JKT imeweza kupanda Hekali mia moja za Mkonge kwa awamu ya kwanza ya mwaka 2021. Naye Kaimu Mkuu wa Kikosi hicho Meja Raymond Mwanry amemhakikishia Mkurugenzi wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa JKT Kanali Peter Lushika kuwa Kikosi chake kitaendelea kuhakikisha malengo ya Serikali yanafikiwa kwa kufuata taratibu zote za kilimo hicho ili kilete tija kama inavyotarajiwa. Aidha Meja Mwanry ametolea ufafanuzi wa Hekali mia moja zilizopandwa kwa mwaka wa 2021 kuwahalikuwa la kuishia Hekali hizo pekee bali ilisababishwa na uhaba wa upatikanaji wa mbegu/miche ya zao la Katani, uhaba huo umekilazimu kikosi kuanza kuzalisha mbegu za mkonge palepale kikosini badala ya kutegemea mbegu za kununua ambazo mara nyingi zimekuwa haziwatoshelezi wadau wote. Kutokana na uhaba huo wa mbegu, Kikosi cha Mgambo JKT kimeandaa shamba la mbegu za Mkonge lipatalo Hekali saba ambazo zitasaidia Kikosi kumudu kupanda shaba jingine la Hekali mia moja zingine na kufanya jumla ya shamba kufikia Hekali 200 ifikapo mwaka 2022. Nao Vijana wa JKT Hamad Shaame na Sophia Chesco, wameelezea kunufaika na mafunzo wanayoyapata kutokana na kushiriki moja kwa moja kwenye Kilimo cha Mkonge, "Tumejifunza mengi kuhusu Kilimo cha zao la Mkonge, Hapo kabla sikujua kama Mbegu ya Mkonge inapaswa kupandwa kwenye vumbi tena wakati wa kiangazi" aliseama Shaame. Akihitimisha maelezo yake, Kanali Peter Lushika amesisitiza kuwa Jeshi la Kujena Taifalitaendele kutekeleza maelekezo ya Serikali kuhusu kilimo cha uzalishaji wa Mazao ya Kimkakakati kupitia Vikosi na Makambi kulingana na mgawanyo wa majukumu uliowekwa.

الفئة

عرض المزيد

تعليقات - 10