ANTHONY KOMU, JOSEPH SELASINI, WILFRED LWAKATARE NA DAVID SILINDE WAFUTWA UANACHAMA CHADEMA
-
Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika amesema Kamati Kuu CHADEMA imefikia uamuzi wa kuwafuta uanachama Mbunge David Silinde na Mbunge Wilfred Lwakatare baada ya Wabunge hao kukiuka agizo la Chama
-
Pia, amesema Wabunge ni baada ya Wabunge hao kujitokeza kwenye vyombo vya habari kutoa maneno ya kashfa na kejeli dhidi ya maagizo ya Chama na Viongozi wa Chama
-
Aidha, amesema Wabunge Anthony Komu na Joseph Selasini pamoja na kuwa wamejipotezea sifa ya uanachama wa CHADEMA, wamefukuzwa baada ya kuendelea kutoa kauli za kejeli, kashfa na kukiuka maagizo ya Chama
-
Mariamu Msabaha, amevuliwa nafasi zake zote ndani ya Chama na kubaki na Ubunge na atatakiwa ajieleze kwanini asichukuliwe hatua zaidi kwa kukiuka maagizo ya chama hicho
#JamiiForums #JFSiasa #Siasa
الفئة
عرض المزيد
تعليقات - 0
مقاطع الفيديو ذات الصلة على ANTHONY KOMU, JOSEPH SELASINI, WILFRED LWAKATARE NA DAVID SILINDE WAFUTWA UANACHAMA CHADEMA - Katibu: