Mgombea urais wa Tanzania kwa tiketi ya CHADEMA, Tundu Lissu, amehutubia umma wa wakaazi wa mjini Mwanza na vitongoji vyake katika mkutano wake wa kampeni kwa kumtaka mpinzani wake kutokea CCM, Rais John Magufuli, kujibu maswali kadhaa yanayohusiana na jinsi yeye na chama chake walivyoendesha nchi kwa miaka yote kabla ya kuomba ridhaa ya kutawala tena kwa miaka mitano ijayo.