Imeelezwa kwamba kadi za kielektroniki za Chama Cha Mapinduzi CCM zitakuwa na mambo makubwa matatu ambayo ni KADI YA BIMA YA AFYA,KADI YA BENKI NA NSSF.
Hayo yamesemwa na Katibu wa NEC Oganaizesheni Issa Haji Gavu alipokuwa akijibu maswali ya wanachama wa Shina namba 7 Kata ya Kising'a Jimbo la Isimani Mkoani Iringa ambapo wanachama hao walitaka kujua kadi hizo zitafika lini.
Aidha amewaambia kadi hizo zitafika kabla ya mwezi wa nane mwaka huu.